New Lyrics

Mbosso – Tamba Magufuli Lyrics

Mbosso - Tamba Magufuli Lyrics
Mbosso – Tamba Magufuli Lyrics

Mbosso – Tamba Magufuli Lyrics Mambo yamepamba moto
CCM chama number one
Kwetu si maneno hapa kazi .
Wapinzani tumbo joto

Kila sehemu wako taabani
Ushindi kwa Magu wazi wazi
Ye nuru sawia uamuzi sifa yake
Uhuru kapinga ubaguzi kwa wanawake

Ye na wala mbuzi hawana chake
Vigeregere viruzi na shangwe kwake

Fungeni maturubai, mkeshe mkisema
Wala hamtupii shida, mkeshe mkisema
CCM twajidai, mkeshe mkisema
Kwetu ushindi kawaida, ooh ooh

Tena Magufuli amekuja na tiba sindano
Acha wateseke
Anachapa kazi baba ye hana mfano
Acha wateseke

Tena ngangari hodari wa mapambano
Acha wateseke
Na tuko na wewe baba mpaka mbili ishirini na tano
Acha wateseke

Tamba Tamba
Tumekupa uwanja tamba
Tamba Tamba
Warushe warushike roho zao

Tamba Tamba
Wenye majipu watumbue leo
Tamba Tamba
Tamba baba nawe

Twaomba akulinde Mungu
Dua zetu sie
Fly Over kama kwa wazungu
Na ndege zetu sie

Na hujatugawa mafungu
Yule na mie
Taifa moja sote kama ndugu
Acha kura tukupatie

Umepambana na Tsunami
La corona lilipoingia
Ni amani kote sasa

Rushwa na unyang’anyi
Tinga tinga umesagia
Mafisadi wote msasa

Hili ndo chama changu nimezama mazima, CCM
Dar ndo jiji langu makonda na lidima, CCM
Makamo wa rais wangu Mama Samia Lima, CCM
Majaliwa waziri wangu katakata mashina, CCM

Fungeni maturubai, mkeshe mkisema
Wala hamtupii shida, mkeshe mkisema
CCM twajidai, mkeshe mkisema
Kwetu ushindi kawaida, ooh ooh

Tena Magufuli amekuja na tiba sindano
Acha wateseke
Anachapa kazi baba ye hana mfano
Acha wateseke

Tena ngangari hodari wa mapambano
Acha wateseke
Na tuko na wewe baba mpaka mbili ishirini na tano
Acha wateseke

Tamba Tamba
Tumekupa uwanja tamba
Tamba Tamba
Warushe warushike roho zao

Tamba Tamba
Wenye majipu watumbue leo
Tamba Tamba
Tamba baba nawe

Tushalinoa panga porini kukata muwa
Yaani tumejipanga wapinzani mtajijua
Tushalinoa panga porini kukata muwa
Yaani tumejipanga wapinzani mtajijua

Tushalinoa panga porini kukata muwa
Yaani tumejipanga wapinzani mtajijua
Lalala lala lalaaaa

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Check Also
Close
Back to top button