New Lyrics

Ferooz Ft Roma – Nalia Lyrics

Ferooz Ft Roma - Nalia Lyrics
Ferooz Ft Roma – Nalia Lyrics

Ferooz Ft Roma – Nalia Lyrics Ukiona mtu mzima analia
Ujue kuna jambo limemsibu
Nimeshindwa kuvumilia
Moyo umepatwa na ghadhabu

Kama tatizo fedha rushwa ningekutolea
Ama ningeweza dhamana ningekuwekea
Lakini imeshindikana chini ya jua
Kama usingizi mauti amekuchukua

Halaumiwi Maulana
Ye anakupenda sana
Kapumzike salama
Kesho tutaonana tena

Hakikwepeki kifo mama
Naamini siku ipo tutaonana
Kifo hakina mwiko wala ujamaa
Na sote tutakwenda kwa Maulana

Kiza kimetanda mwanga mshumaa
Huzuni imetawala furaha imesinya

Nalia kutoka moyoni
Kukuona tena natamani
Nakuchomea na ubani
Mola akulaze peponi

Nalia kutoka moyoni
Kukuona tena natamani
Nakuchomea na ubani
Mola akulaze peponi

Ndo ameshalala huyo haamki
Hata mmshikie bunduki hatokaa
Hatwafaa, ila roho yake itapaa
Ndo maandiko yanavyosema
Maana huwezi tena kwema
Japo ametuacha mapema dah

Sasa amkeni muageni
Mumpe heshima za mwisho
Maana hamtomuona tena
Na pia mpate fundisho
Hiki ni kifo sio sinema

Na aliyezaliwa na mwanamke
Siku zake zinakwisha
Sasa basi sote tuinuke
Tujiandae kwenda kumzika

Loka ashaingizwa kwenye mwandani
Na si tushauchoma ubani
Basi turudi nyumbani
Huku tukitafakari baada ya ye atafuata nani

Labda wewe
Basi swali usingoje uswaliwe na watu
Kaburini utakuwa mwenyewe
Ukiongoja malaika wa wafu

Nanyi mnaoshika chepe
Kumfukia mwenzenu
Siku nanyi mtafikiwa itakapokata pumzi yenu
Sasa msisite msiogope
Mkaacha kumzika mwamba mkachimba
Mbinguni hauingiii na kope
Sasa iweje unavimba

Unadharau wenzako
Kwa jeuri ya madaraka
Na kwa kiburi cha cheo
Unawatoa wenzio sadaka
Kwa umaarufu wako wa leo
Unatuona si taka taka
Kwa pesa zako na mkeo
Unakosa utu unanata

Haya si ulimchukia marehemu
Leo hayupo tena duniani
Unatamani aamke umuombe msamaha
Na haiwezekani
Ikiwa umezaliwa makongo
Ukipinga kifo hauwezi
Sote tutarudi kwenye udongo

Kiza kimetanda mwanga mshumaa
Huzuni imetawala furaha imesinya

Nalia kutoka moyoni
Kukuona tena natamani
Nakuchomea na ubani
Mola akulaze peponi

Nalia kutoka moyoni
Kukuona tena natamani
Nakuchomea na ubani
Mola akulaze peponi

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button